#NEWSMICHEZO : Pirlo: Mashabiki Wa Liverpool Timizieni Wajibu Wenu Kwa Balotelli

Kiungo mkongwe kutoka nchini Italia Andrea Pirlo amewataka mashabiki wa klabu ya Liverpool kupunguza munkari dhidi ya mshambuliaji Super Mario Barwuah Balotelli kutokana na kiwango anachokionyesha tangu aliposajiliwa huko Anfield.
Pirlo ambaye ni kiungo wa klabu bingwa nchini Italia Juventus amesema hakuna haja kwa mashabiki wa klabu ya Liverpool kumnyooshea vidole mshambuliaji huyo na badala yake wanatakiwa kuwa wastahamilivu na kutarajia mazuri kutoka kwake.
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 37 amesema kwa kipindi cha miaka kadhaa alimfahamu Balotelli na jambo kubwa alilolibaini kwa mshambulaiji huyo ni kuhitaji kupewa nafasi na kuonyeshwa upendo katika jamii inayoishi nae.
Amesema kinachokosekana kwa mashabiki wa Liverpool dhidi ya Mario Balotelli, ni kukosekana kwa mapenzi baina ya pande hizo mbili na mwishowe mambo yamekuwa yakienda mrama ndani na nje ya uwanja.
Amesema endapo Balotelli atapewa nafasi na kuonyeshwa upendo na kila mmoja huko Anfiled atafanikisha azma ya kucheza soka safi na kufunga mabao kama inavyohitajika na walio wengi.
Super Mario Barwuah Balotelli amecheza mara kadhaa na Andrea Pirlo katika kikosi cha timu ya taifa ya Italia tangu mwaka 2010 na tayari amecheza michezo 33 na kufunga mabao 12 akiwa na mabingwa hao wa dunia wa mwaka 2006.
Balotelli alisajiliwa na klabu ya Liverpool majira ya kiangazi akitokea nchini kwao Italia kwenye klabu ya AC Milan kwa ada ya uhamisho wa paund million 16 na tayari ameshacheza michezo kumi akiwa na klabu hiyo ya nchini Uingereza huku akifunga bao moja.
Share on Google Plus

About IF YOU DON'T KNOW NOW YOU KNOW

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment